BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Monday, July 20, 2009

WAGOSI WA KAYA NA TANGA KUNANI...!! JAMAA WAPO KIMYA SANA JAMANI


Kwa wale ambao wamekuwa wafatiliaji wakubwa wa muziki wa bongo flava nchini Tanzania, hakika watakuwa wanawafahamu WAGOSI WA KAYA- vijana mahiri wa muziki huo kutokea hapa jijini Tanga.


Kwa hakika walibamba sana na staili yao ya ki'lugha....kwa maana ya kisambaa na kidigo, hawa wa Dr John na mwenzake Mkoloni. Unakumbuka ngoma zao kama TANGA KUNANI, WAUGUZI, TRAFIKI HAYAAAA!!, KEROOO, SOKA LA BONGO na nyengine kibao tu!!


Baada ya kukumbuka nyimbo hizo, jiulize ni kiasi gani zilikubamba na je sasa hivi wapo wapi na wanafanyanini...!!??? Ukimya wao umeonekana kuwagusa watu wengi ambao kwa namna moja ama nyenigne walikuwa tayari wameshazama kwenye dimbwi la upendo wa nyimbo zao ambazo zilikuwa zinagusa moja kwa moja jamii ya kitanzania.


Kwa hapa Tanga jamaa walikuwa kama akina P Square wa kule nchini Nigeria, si mtoto wala mkubwa- kila kona utasikia TANGA KUNANI kama vilivyo VIJIMAMBO VYA TANGA kwa sasa. Duh....jamani mmekaa kimya sana wagoshiiiii, tunaomba mrudi tena ili tufurahie tena ladha zenu za kisambaa na kidigo.


HAYA NI MASHAIRI YA WIMBO WA TANGA KUNANI!!
Wagosi wa Kaya - Tanga kunani?


(verse 1)Tanga kwa kweli ni kijimji kidogo, na pia kuna mambo ya uswahili si kidogo. lakini habari zake kwa kweli ni kubwa, na mji ule ukiuvamia kwa papara palee, mengi yatakukumba! Ukifika Tanga utatambuaje kama kweli huu nd'o mkoa wa Tanga?Utaona wanawake wengi palewamejifunika mabaibui na vijikanga. Waume makanzu baraghashia, mkononi tasibihiwanakuhesabia.
Baiskeli ndiyo teleeee, mpaka zawakera wenye magari barabaraniHalafu hali ya sasa sii kama ile yazamani, ukaenda ovyo tu utauza kila kitu chako cha thamani.Matajiri wa enzi zile ukiwaonaleo hii tena hawana thamani Enzi zile bwana mkoa wa Tanga kilakitu mambo yalikuwa swafi. Mijikazi ilikuwa tele, na kulikuwa hakuna mambo yaukorofi, lakini sasa hivi thubutu, twendelea kuchakaa mpaka tutoke ukurutu, hakuna ndimaa, kilo mtuambiwa ajifanya mvuvi ati, na ukamshauri mtu akushushia varangati, astaghafirullai laadhim!Watu waongea peke yao kamavile wendawazimu, labda tutambikemizimu huenda kidogo pale mamboyakany'oka. Palikuwa na viwanda na mashamba ya mkonge telee. Haviwapi sasa? Utafikiri mamiye mwali aliyefunga kizazi bwana, maana havizalishi ati, vyote viko, nyang'anyang'a. Hali hii kutupa vitu njia panda, yaonyesha kabisa tayari maisha yeshatushinda. Watu kilo siku waenda kwa waganga, ukipita pale mara kumevunjwa nazi, mara huku nako kule kumetupwa hirizi, mwatakani basi nyiye wana msiotulia?


KIITIKIO



Tanga, kunani paleee, mbona kila kitu pale kimekufa, Tanga, kunani paleee, mbona maisha pale yanasikitisha.
(verse 2)lshi Tanga lakini kuwa makini,watu wajua mpaka siri zako za ndani, sijui habari hizi huwa waambiwa na nani?
Hospitali ya Bombo ya leo ni vichekesho,ukienda pale hata kama utumbo uko nje, utaambiwa tu matibabu kesho. Tanga, Tanga jamani yarabi toba.Ndege pia kwa mwezi twaona mara moja, basi balaa hili watu tumekuwa twaishi maisha yatumbiri, sijui tusomeane alubadili,ili tumkamate alotu filisi utajiri.Bandari nayo sasa yachungulia shimo, zamani waweza ona miji meli palee wala haina kipimo, lakini! sasa hivi si meli tena, wala hazina uwezo wa kubeba hata kontena. Ukiondoa Wahindi na Waarabu, Waswahili wenye pesa ni wa kuhesabu, halafu wikiendi angalia nyendo zao, kuchukua wake za watu na kutaka mambo nje ya uwezo wao.
Saruji ndo kiwanda arnbachokimebakia, panga pangua makaburu wameingia ubia. watafanyabiashara miaka mitano haifiki nao wale pia watajiondokea
Railway kimyaa, zamani wenyewepale tulishaizoea mijihoni, sasa hivibehewa moja la abiria hatulioni,mwawekani basi mabehewayaloozana pale. Si muondoe jamayaleta mafico wezi yale.


KIITIKIO



(verse 3)Hatijawahi kulalamika sisi hatasiku moja,najuu ya maisha ya Tanga MC natoa hoja, msije mkaona mzaha jamani hivi si vioja, kucheka mtacheka lakini mkoa unadodaViongozi wetu kazi yao hawajui hata moja, vikao vyao n'vingi wanakutana Mkonge Hotei,na agenda za huko hawatiambii ukweli.
Promise zao ni za uongo haziambiiki, sijui wametuona mma'bahau ama m'visiki,Tinapomichagua majukumu yenu mnayatambua? Au mnaona raha dada zetu kuuza vitumbua?
Titabeba zege mpaka lini na kujitutumua? Inaelekea mmetisahau halafu pesa mnazitumbua.Na huu mpango mpango wa Tanga wa vipande vya baiskei,titakuja kutoana roho mchana mchana aisee, tinashikwa na mgambo ili tilipie manispaa, wakati wagosi wa kaya wenyewe ti nakufa na njaa. asalam alekum wallahiNdio maana akili zetu mnasema hazifai, na asubuhi ni mnazi badala ya chai.Pamoja na viwanda na upuuzi huo kufa, elimu tinaichezea halafu kingereza n'cha ugoko. Tisibishane hapoo!Sasa tirudi katika suala ya maendeleo, tinapataje mtaji kwa ajili ya haya maendeeo? Kama si kupakiza magunia kwenye Shengena, tinalipwa hela kidogo haafu tinasengenywa.Chai asubuhi ni kavu hakuna cha kutafuna, watoto wamezoea ubwabwa siku huna hela wananuna,
Wake zetu wamekakamaa utadhani wanafanya diet, haku nacha diet hapo ukapa umepanda chatiNa ukitaka kujua n'balaa kwa haya tinayosema,uwanja wa sabasaba umekufa, hata jumba ya sinema.Msije mkani kumbusha mimi hapa naweza kulia.Oh Tate none wa Tanga tushikamane.Mike Byanaku ni fundi mzuri wa baiskeli, anasaidia sana lazima niseme ukweli. Anapogonga nyundo Wahindi wanasema n'kelele,nntafutieni nyundo yasailensa aondoe hizo kelele.
Na nyie na magari yenu msipige honi wala misele, hapo titaelewana.Tanga tina barabara maarufu na ziko ishirini na moja, na hizi zimejipanga panga na ni hatari kwa vioja, tega sikio usikie ni kitu gani kinakuja.
Tinao akina kaka wanaoshikishwa ukuta, wengine wanajifanya waswalihina wanakula kitimoto, hatiwasemi tinaogopa mkong'oto.Tanga Wahindi wamejazana kwenye maghorofa ya msajii,tunabaki kuhangahanga Kwanjeka sisi waswahii, ukipita chini ya ghorofa wanakutemea mate ya palikiUkiuliza hivi n'kwa nini matusi yake hayaambiiki. Weee Master J!Kuna siku n'tampandia mtu ghorofani nimtoe roho, halafu n'pelekwe kwenye gereza la Maweni n'kanyee ndoo.Timeshachanganyikiwa mnatiletea ubishoo.Juhudi zako zinaonekana sana Kapteni Mkuchika. Afadhali sasa kidogo Tanga tinahema na kucheka.Maneno tinayoongea hapa hatumpigi mtu kamba, Wagosi tinamalizia na salamu kwa Makamba.Baba yetu Makamba, hawa akina matonya hawako tu pekee Daisaama, hata kule Tanga wamejazana ni kiama.


KIITIKIO


No comments:

Post a Comment