BLOG HII IMEDHAMINIWA NA: MWEKASU HOSTEL, PWEZA NIGHT CLUB TANGA, SOPHIA PRODUCTION, AFRICAN DESIGN, BREEZE FM, PANGANI COAST CULTURAL TOURISIM PROGRAMME, NA SAFARI LODGE ANNEX
Photobucket

Tuesday, March 31, 2009

MISS TANGA CITY CENTER MWAKA 2009

Anaitwa Zena Kassim, ni mmoja kati ya wakurugenzi wa Miss Tanga City Center.

Huyu anaitwa Fatuma Makoko, nae ni mkurugenzi wa Miss Tanga City Center.
Kwa pamoja ndio wanaunda ZEFA Promotion, ambayo ndio inasimamia Miss Tanga City Center kwa mwaka wa 2009

Hapa wakiwa na wasimamizi wengine wa mashindano hayo ambayo kwa pamoja wamedai kumtoa Miss Tanga na hata Miss Tanzania. Kulia ni Don Chill na aliyesimama kushoto ni Khaleed.


Ukisikia Tanga Raha ndio hii, huyu anaitwa Pili Miraji ni mwalimu wa walimbwende wanaowania taji la Miss Tanga City Center


Umeshawahi kusikia SOFIA PRODUCTION..? Huyu ndie mmiliki wake, anaitwa Aisha Kisoky- Ndie mdhamini wa mashindano ya Miss Tanga City Center

Mama Sofia Production akiwa na mmoja wa wakurugenzi wa mashindano ya kumsaka mrembo wa Miss Tanga City Center


SASA WATAZAME WAREMBO WAO



Anaitwa Leyla Issa. Umri wake miaka 18, ni mshiriki wa Miss Tanga City Center mwaka 2009

Anaitwa Salome William. Umri wake ni miaka 18, ni mshiriki wa Miss Tanga City Center mwaka 2009


Anaitwa Agnes Sambo. Umri wake ni miaka 21, ni mshiriki wa Miss Tanga City Center mwaka 2009



Anaitwa Rachel Mlaki. Umri wake ni miaka 20, ni mshiriki wa Miss Tanga City Center mwaka 2009


Anaitwa Martha Moses. Umri wake ni miaka 18, ni mshiriki wa Miss Tanga City Center mwaka 2009


Anaitwa Neema Komba. Umri wake ni miaka 19, ni mshiriki wa Miss Tanga City Center mwaka 2009

Anaitwa Ester Flavian. Umri wake ni miaka 19, ni mshiriki wa Miss Tanga City Center mwaka 2009

Monday, March 30, 2009

HUYU NDIYO HANDSOME WA TANZANIA.


Hivi majuzi pale New Africa Hotel jijini Dar-es-salaam,palifanyika shindano la kumsaka The Most Handsome Man in Tanzania au ukipenda Mr.Bongo kwa mwaka 2009. Jumla ya vijana 11 walifikia fainali hizo ambapo mshindi aliibuka kuwa Khalid Mohamed(pichani).
Mshindi huyo ambaye bila shaka ndio ashaanza kuingia katika lile kundi la “umaarufu”,alijipatia zawadi ya US $ 1000 na shopping ya uhakika katika maduka ya Zizzou Fashion.
Majaji wa shindano hilo walikuwa Steven Kanumba, Christina Isabbela na Richard ambaye alikuwa mshindi wa Big Brother 2007.

Friday, March 27, 2009

Mh. Mohammed Abdulazizi- Mkuu wa mkoa Tanga.

MKUU wa Mkoa wa Tanga,Mheshimiwa Mohamed Abdulaziz akizungumzia maandalizi ya zoezi la upigaji kura za maoni kuwaibini watu wanaojihusisha na Mauaji ya Albino,Vikongwe na wanaojihusisha na vitendo vya ujambazi pamoja na uuzaji na ununuzi wa dawa za kulevya katika kipindi cha Amka na Mwambao Machi.27.2009.
Zoezi la upigaji kura huo limefanyika Mkoani Tanga Machi 28 mwaka huu ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Waziri Mkuu,Mheshimiwa Mizengo Pinda aliyelizindua Machi 5 mwaka huu.
Anayefanya mahojiano naye ni Msimamizi wa Kipindi cha Amka na Mwambao kinachotangazwa na Radio Mwambao FM 106.0 cha jijini Tanga,Bw.Benedict Kaguo
.


Kipindi cha Amka na Mwambao hujadili masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na Kero za wananchi,Mada mbalimbali ambazo msikilizaji hupata fursa ya kupiga simu ama kutuma ujumbe mfupi wa maandishi kuuliza ama kuchangia mada hiyo.
Kipindi kinarushwa kila siku za isipokuwa Jumapili kuanzia saa 12 asubuhi hadi saa 3 asubuhi na kinadhaminiwa na Mtandao wa Simu za Mkononi wa Tigo.

Unapokuwa Mkoani Tanga sikiliza kipindi hiki kupitia 106.0 Mwambao Fm Sauti ya Tanga uweze kuhabarika na kuburudika zaidi.


Katika Kipindi hicho watu mbalimbaliwameshahojiwa akiwemo Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga,Simon Sirro,Mkuu wa Wilaya ya Mkinga,Bw.Deodatus Kinawiro,Afisa Uhusiano na Umma wa Mamlaka ya Majisafi na Maji Taka jijini Tanga,Tanga Uwasa,Muuguzi Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Tanga Bombo,Dokta Joseph Nzige,


Pia Mkuu wa Kikosi cha Zimamoto jiji la Tanga,Ayubu Mhando,Mratibu wa Elimu ya Sekondari Wilayani Mkinga,Omari Kombo,Mwenyekiti wa Halmshauri ya Wilaya Mkinga,Zahoro Idrisa,Katibu Mkuu wa Coastal Union,Salim Bawazir,Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Kikapu Mkoa wa Tanga,Hamisi Jafari,Katibu wa Uhamasishaji wa Mchezo wa Ndondi Mkoa wa Tanga,Allan Kamote.




OMEGA BOYS KUTOKA NA ALBAMU MPYA


HAWA NDIO VIJANA WA OMEGA BOYS


MTU MZIMA KOCHAS AKI'SHOW LOVE KWA WADAU



HAPA WAKIWA LIVE NDANI YA STUDIO ZA MWAMBAO WAKIFANYA INTERVIWE NDANI YA KIPINDI CHA THE HOT BEAT




BRA-A AKIWA MZIGONI WAKATI AKIWAFANYIA INTERVIEW VIJANA WA OMEGA BOYS, NYUMA NI DJ ROGGER KISS



HAPA NIKIWA NA DJ ROGGER KISS TUKIFUATILIA INTERVIEW KWA MAKINI



AMANI KWENU WADAU WANGU WOTE WA JIJINI TANGA NA KOTE AMBAPO MNANISOMA






Thursday, March 26, 2009

MTU MZIMA HAPA WAKATI NIPO MZIGONI-ANKO MO


MSG ZA MAPENZI KWA WADU WANGU
1. Natafuta ni jinsi gani naweza zifikisha zangu hisia, moyoni nazidi umia kwa jinsi nilivyokuzimia, nakupenda my dear!
2. Siku zote moyo wangu umekuwa ukiangaika ukitafuta hifadhi yaw uhakika, hakika kwako umefika, nakupenda fika.
3. Hakika moyo wangu umeuteka, kwako najiona kama mateka, chochote unachotaka, hakika kwangu utapata, luv u.
4. Wewe ndio wangu wa dhamani uliyopo kwenye yangu ramani, kwa mwingine sitaweza kwenda maanani, nakupenda.
5. Najiona kama mfungwa nisiye na hatia tangu penzi lako uliponipatia, nakupenda my dear.
6. Nakupenda na daima nitakuenzi siku zote nitakazokuwa chini ya jua na mwezi, amini kwa mwingine kwenda siwezi!
7. Hakika nilikupenda na wazi nilijua kwako nimefika kumbe najidanganya na zangu fikra, sikuhitaji tena kwenye yangu himaya.
8. Nilikupa hadi visivyohadithika nikiamini hayo ndio mapenzi ya uhakika, lakini kiumbe hukulidhika, penzi langu hutapata daima fika.
9. Wangu mpenzi unayejua kunienzi tangu enzi za uchumba hadi ndoa, mchana umefika nahakika njaa imekushika tumia japo nusu dakika upate mlo wa uhakika, nakupenda.
10. Wewe ndio wangu tabibu unayejua haswa kunitibu, wengi hivi leo wanionea wivu, daima nitakutunzia zako mbivu uzile taratibu, nakupenda.

MFAHAMU MISS TANGA ANAYEMALIZA MUDA WAKE.

NADYA MOHAMMED


Hapa akiwa na mkoko wake




Hapa akiwa na shungi


Cheki mtoto alivyopiga Mini!!



Wednesday, March 25, 2009

MOJA KATI YA MA'DJ WAKALI JIJINI TANGA- DJ BOB NASS



Nikiwa jijini Tanga nilikwenda disko usiku katika club moja maarufu jijini hapa inayoitwa Lacasa Chica. Kulipigwa nyimbo changanyiko na zakuvutia sana, muda wote huo nilikuwa kwenye kiti nikipata kinnywaji. Ila ulipoigwa wimbo wa Lady uliopigwa na vijana wa Modjo wanaotokea kule nchini Ufaransa nikashindwa kuvumilia.


Hakika ulikuwa wimbo mzuri sana ulionivutia na kugusa hisia zangu. Hivyo ilinibidi niinuke toka kitni na kwenda kuselebuka, baada ya muziki huo kuisha ndipo nikaamua kwenda juu aliko Dj anayepiga muziki ili nimpongeze kwa kazi nzuri.


Nilistaajabu baada ya kumuona kijana mdogo kiumri hadi kiumbo nikidhani labda kamshikia Dj husika. Sikusita kumuuliza maswali machache, na ndipo nilipogundua kuwa ni yeye ndiye aliyekuwa akiporomosha muziki kwa kipindi chote kile nilichokuwa pale.

Nilishtuka sana!!
Kikubwa kilichonishtua ni kutokana na umahiri wake wa kufanyanya "Scrutching" pamoja na kupangilia midundo ya muziki aliokuwa akipiga. Hakika sikuwa mimi pekee niliyevutiwa na utundu aliokuwa anaufanya, nilishakuwa na mazoea ya kusikiliza muziki bila kufanyiwa "Mixing"- au hata kama ikiwa hivyo basi ni kwenye Redio ambazo zina watu ambao wamesomea kwa kina maswala hayo.


Nikapata hamasa ya kufanya nae mahojiano si unajua kazi zetu za uandishi ni kama askari akiwa vitani kila unapoenda unakuwa na zana tayari kwa lolote, mahali popote bila kujali mazingira ili mradi hali iwe ina ruhusu.

Akiniambia nimpe kama nusu saa aweze kumaliza kazi kisha tuongee nami kwa vile nilikuwa natamaa ya kujua kwanini kijana kama yeye baada ya kuwa anajisomea kwa muda huo wa usiku yuko mahali kama pale anaburudisha watu.
Kwa zile nusu saa alizonipa, zilikuwa pia changamoto kwangu kuweza kumsikiliza kwa kina ili ninapoanza nae mahojiano nipate kitu ambacho nimekikusudia kukipata toka kwake.


Nilijivuta pembeni karibu na kinywaji changu nilichokuwa nimekiwacha mezani, kisha nikawa nasubiri.
Alipomaliza ndipo sasa Tukaanza mahojiana kwa kunafahamisha yeye ni nani na anatokea wapi. Jina lake la kuzaliwa ni Nasir Bakari Thabit, ana umri wa miaka 20 na kabila lake ni Mngoni. Pamoja na kutokea Iringa lakini pia kijana huyu ni mwenyeji wa mji wa Tanga kwani amezaliwa hapa na kusomea hapa pia.
Anasema alianza masuala ya muziki toka akiwa shule ya msingi darasa la nne, wakati huo alikuwa anapenda sana kusikiliza muziki wa rap haswa wa msanii mongwe kwenye ramani ya Bongo Flava hapa nchini Tanzania Joseph Mbilinyi maarufu kama Mr2.


Zaidi ya hapo pia alikuwa akimhusudu sana hayati 2pac Shakur na alikuwa akiyaandika mashairi ya nyimbo za wasanii hao pembeni kitu kilichofanya ajue kuimba kwa kufuatisha mashairi na akaanza kujifunza utunzi akiwa na umri mdogo.
Alipofika darasa la tano alikuwa anaufahamu wa muziki huku akiwa na mjomba wake anayeitwa Musa Thabit ambaye alikuwa anakwenda nae disko toto wakati wa likizo. Wakifika disko yeye na mjomba wake wanakaa kwa Dj kisha mjomba wake anamuomba Dj amfundishe Nasir jinsi ya kupiga muziki na vitu vidogo vidogo vinavyohusiana na u'Dj.

Kutokana na mwanzo huo aliweza kujijenga vyema na kuweza kupiga disko kwenye madisko toto mbalimbali yaliyokuwa yanafanyika wakati huo kama vile Saruji club pamoja na Maweni club hasa wakati wa sikukuu na likizo ndefu.
Alipoingia sekondari mwaka 2004 tayari alishajua mambo mengi kuhusu maswala ya muziki na u'Dj kwa ujumla kwani alikuwa anakwenda Internet Caf'e kujifunza zaidi na kujua watu wa nchi za magharibi wanafanya nini kwani kwa hapa Tanzania hakuna shule ya u'Dj na kupitia Internet alidhanin kungeweza kumsaidi.


Aliweza pia kufanya Downloading kwa softwares za u'Dj ili kufahamu vizuri na pia wakati wote huo akiwa shule, rafiki zake walimtia hamasa na hari ya kujifunza zaidi muziki na u'Dj ambapo hadi anamaliza kidato cha nne tayari alikuwa ni mzoefu juu maswala hayo.
Mnamo mwaka 2008 alifanikiwa kuingia katika kituo cha radio hapa jijini Tanga kinachoitwa Mwambao fm. Hapo Nasir alijifunza si tu u'Dj bali hata uandishi wa habari na utangazaji.
Akiwa Mwambao Fm tayari amekutana na watu wengi waliokuwa na ufahamu zaidi yake na kwamba mpaka sasa anapiga kwenye kumbi mbalimbali mmoja wapo ndio ambao alikutana na mwandishi wa makala hii.


Nasir au Bobnas anasema katika kuhangaika kwake kulikuwa kuna watu waliokuwa wakimpa moyo na kumuongezea hari kwa kila hatua anayoifikia. Akiwashukuru watu hao, Bob Nas aliwataja wazazi wake pamoja na familia yake kwa ujumla, mjomba wake, marafikizake na pia Mkurugenzi wa radio Mwambao Bw Ahmed Simba kwa kukiona kipaji chake mapema na kukiinua halikadhalika Dj maarufu kwa mkoa wa Tanga Raphael Chambo au Dj Rach kuty na Dj Donchlee ambao bado wanaendelea kumpa mafunzo zaidi.
Hata hivyo Nasir ndoto zake ni kuwa mmoja wa maDj maarufu kama vile John Dilinga au Dj JD ambaye kwa upande wake anamkubali kwa kazi zake, ambazo kwa upande wake zimekuwa zikimpa changamoto sana.


Pia kuhusu swala la kuwa producer, Bob Nas maarufu kama Mkali wa milazo- mchai wa Mixing amesema kuwa kwa sasa ameanza kujifunza kuhusiana na utengenezaji wa nyimbo.

Pamoja na kutaka kutema cheche kwenye maswala ya utengenezaji muziki, Nasir pia ameshawahi kushirikishwa kwenye wimbo wa msanii maarufu kwenye muziki wa Bongo Flava anayeitwa Pete ambaye pia ameshawahi kutamba na kibao chake cha Mazoea alichomshirikisha Rado.
Wimbo ambao Nasir ameshirikishwa na msanii huyo unaitwa Nenda ambao pia ndani yake kuna Dj Roger Kiss ambaye nae ni mmoja kati waonafanya vizuri Redio mwambao pamoja na Tin Dady, kazi ilifanyika King Falcom Production chini ya Producer Sam Chad.
Huyo ni Nasir Thabit, wengi humfahamu kama Dj Bobnas. Kwa sasa ni mmoja kati ya wafanyakazi wa redio Mwambao Fm, ambayo ipo hapa jijini Tanga.

Safari yake yakulekea kwenye u'Dj bora na u'Producer ni ndefu sana, ila amenipa changamoto kuwa kama wazazi tunapaswa tuangalie watoto wetu wanataka nini na tujaribu kuwapa moyo na tushirikiane nao kwa pamoja katika kutimiza ndoto zao kwani kama sio mjomba wake kukiona kipaji chake toka hapo awali basi nafikiri sasa hivi angekuwa darasani akipata elimu. Sipingi asisome, ila kipaji ndio kitu pekee kilichomfanya awepo mahala alipo sasa.
HII NDIO RAMANI YA TANGA WADAU WANGU

Tanga google satellite maps
KITU GANI KILICHOMKIMBIZA DUNGA TZ..?


Ambros nkwabi aka dunga arejea nchini kwao baada ya miaka mitatu mfululizo ya kazi zake dar-es-salaam.nimerejea kenya na tayari nimeshaanza kazi mimi na kaka yangu shaky tumeshaanza kuwa busy na kazi za wasnii wa hapa.


Amesema dungalakini wadau wengine wanadai kuwa dunga ameondoka nchini baada ya work permit kuisha muda na kukabiliwa na vipingamizi kutoka serikalini kuhusu kuongeza muda wa work permit yake.


Work permit ya dunga iliisha muda miezi kadhaa iliyopita na alishindwa kuongeza muda wake baada ya wahusika kukataa ombi lake habari zaidi alizitoa akidai kutokutajwa jina lake.source huyo aliendelea kusema kuwa producer huyo wa kikenya alileta tishio kubwa kwa wapinzani wake kibiashara na kuteka show zote kitu ambacho hakikuenda sawa kwa upande wake yeye.


Wengine walikuwa wakimpinga mpaka kufikia hatua ya kutoa rushwa ili work permit yake isiongezwe mudadunga hakusema chochotekuhusiana na hayo.
CHEKI VITOTO VINAVYOPIGA MBIZI- KUDADADEKI, OLE WAO HAPA ATOKEE LUBA!!


MOJA YA BLOG ZINAZOFANYA VIZURI MITANDAONI- HABARI NDIO HIYO

Tuesday, March 24, 2009

NAKAAYA NDANI YA LUV NA M1 WA Dead Prezz
Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya Nakaaya Sumari ambaye siku za karibuni wametemana na mchumba wake wa siku nyingi, hatimaye amezama ndani ya penzi zito la msanii wa kundi la Dead Prezz kutoka Marekani M1. M1 ambaye ameshirikishwa kwenye...Mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya Nakaaya Sumari ambaye siku za karibuni wametemana na mchumba wake wa siku nyingi, hatimaye amezama ndani ya penzi zito la msanii wa kundi la Dead Prezz kutoka Marekani.M1 ambaye ameshirikishwa kwenye wimbo wa Mr Politician ulioimbwa na mnyange huyo.Katika mahojiano na kituo kimoja cha Radio kipindi yupo nchini M1, akiulizwa swali la kizushi M1 aliwahi kukiri kuwa Nakaaya ni mwanamke mrembo ambaye mwanaume yeyote akiambiwa awe nae hata sita kukubali na kama hatakubali basi atakuwa na matatizo.Baada ya majibu hayo ya M1 yalizuka maneno ya kuwa baada ya Nakaaya kuachana na mchumba wake wa siku nyingi alikuwa na mahusiano na Mwanamuziki huyo habari ambazo zilikuwa za chini ya kapeti mpaka leo hii ambapo Nakaaya kwa mdomo wake mwenyewe amekubali kuwa ni kweli ana uhusiano na msela huyo wa nchini kwa Obama.Akipasha zaidi Nakaaya anasema kuwa tayari wameshaingia kwenye hatua za kuelekea kwenye agizo la Mungu yani kufunga pingu za maisha kwani jamaa tayari kashamvalisha pete ya uchumba hivi karibuni.

Tuesday, March 24, 2009

Mfahamu Ricardo Kaka Kwa Undani

Ricardo Izecson dos Santos Leite "KAKA"- MLOKOLE ANAYETANGAZA INJILI KWENYE SOKA.

Kama utazungumzia wachezaji ambao wamepata mafanikio zaidi kwenye ramani ya soka duniani, hasa kwenye timu ya taifa ya Brazili na klabu ya Ac Milan ya nchini Italia. Basi hutasita kumtaja mshambuliaji Ricardo Izecson dos Santos Leite, wengi humfahamu kama 'Kaka'.
Alizaliwa mnamo April 22 mwaka 1982 huko nchini Brazili kwenye mji mkuu wa nchini hiyo Brasilia. Ni mshambuliaji mwenye umri wa miaka 26 kwa sasa, na pia ana urefu wa futi 6.
Kwa sasa mchezaji huyo anachezea klabu ya Ac Milan ya nchini Italia akiwa anavalia jezi namba 22. Kipaji chake kilianza kuchomoza akiwa na timu za vijana wadogo wakati huo akiwa na miaka minane tu.
Pia alikuwa akicheza na vijana wenzake katika klabu ya Sao Paulo hata kufanikiwa kuwamo katika kikosi cha pili na alipofikia umri wa miaka 15, alisaini mkataba na kikosi cha vijana wa SPFC kwa ajili ya michuano ya Copa de Juvenil.
Kutokana na kiwango chake, mwaka 2001, Kaká alipandishwa katika kikosi cha kwanza na kufanikiwa kutikisa nyavu mara 12 katika mechi 27, hivyo kuwa mfungaji bora wa São Paulo na kuibebesha ubingwa.
Katika msimu uliofuata, Kaka alifanikiwa kupiga bao 10 kwenye mechi 22 za ligi hiyo na ndipo hapo alipoanza kutakiwa na klabu kubwa barani ulaya.
Klabu ya AC Milan, ikiwa bingwa wa ligi kuu ya Italia msimu wa mwaka 2003, ndipo ilipoamua kumnunua Kaka kwa kitita cha dola mil. 8.5 za Marekani kwa mapendekezo ya mmiliki wa klabu hiyo, Silvio Berlusconi.
Punde tu alipotinga kwenye kikosi cha timu ya Milan, Kaka alionekana kuwa na hamasa kubwa ya mafanikio kwani katika mechi ya kwanza ya ligi kuu nchini humo maarufu kama Serie A- Ac Milan iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ac Ancona.
Kuhakikisha kuwa uwezo wake ni mkubwa kisoka, hadi mwisho wa msimu huo- Kaka aliweza kuondoka na mabao 10 kwenye mechi 30 alizocheza na hatimae kuibebesha kombe la Scudetto klabu yake hiyo halikadhalika ubingwa wa Super Cup barani ulaya.
Aidha, Kaká alikuwa miongoni mwa washambuliaji watano wakali kwenye msimu wa mwaka 2004/2005, akiwa nyuma ya kinara wa mabao wa msimu huo, Andriy Shevchenko.
Zaidi ya hapo mchezaji huyo pia alifunga mabao saba katika mechi 36 kwenye ligi ya Serie A, wakimaliza kwa kuwa nyuma ya Juventus.
Kwa msimu huo huo wa mwaka 2004/05, Ac Milan ilipata pigo kwa kushindwa kutwaa ubingwa wa Ligi ya Ulaya kwa kufungwa kwa mikwaju ya penati na timu ya Liverpool ya nchini Uingereza.
Hata hivyo, pamojana na Ac Milan kukosa ubingwa huo, Kaka aliweza kuchaguliwa kuwa mshambuliaji bora wa mashindano hayo na kumaliza msimu huo kwa kutwaa tuzo ya Ballon D’Or.
Msimu uliofuata wa mwaka 2005/2006, Kaka aliipigia timu yake mabao matatu kwenye mechi moja yaani 'Hat-Trick kwenye mashindano ya nyumbani.
Aprili 9, 2006, aliifungia tena mabao matatu klabu yake dhidi ya Chievo Verona. Mabao hayo aliyapiga katika kipindi cha pili cha mchezo.
Baada ya Shevchenko kuikacha klabu hiyo na kuchukuliwa na klabu ya Chelsea ya nchini Uingereza, msimu wa mwaka 2006/2007 ulionekana bora sana kwa mchezaji Kaka baada ya kuweza kumudu nafasi ya kiungo na mshambuliaji.
Msimu huo huo ulimalizika kwa mchezaji huyo kuwa mfungaji bora wa ligi ya mabingwa barani ulaya maarufu kama Uefa Champions League huku akiiwezesha timu yake kutwaa ubingwa wa michuano hiyo migumu barani humo.
Hata hivyo moja kati ya mechi ambazo zimebaki kuwa ni historia nzuri kwa mchezaji huyu, ni ile dhidi ya Manchester United ambapo ilimlazimu kocha wa timu hiyo Sir Alex Ferguson kumpa pongezi kocha wa Milan Carlo Ancelotti baada ya timu yake kuisambaratisha United kwa jumla ya mabao 3-0 kwenye nusu fainali ya klabu bingwa barani ulaya.
Pongezi hazikumfikia kocha wa timu hiyo pekee, aidha Ferguson alikiri kuwa Kaka, ni miongoni mwa wachezaji bora kwenye ramani ya soka duniani kwa mwaka huo.
Kilichofuata baada ya mechi hiyo, ni Kaka kutajwa kama mchezaji bora wa dunia na jarida la michezo la Italia, liitwalo Gazzetta dello Sport.
Juni mwaka 2008, gazeti la michezo la nchini Ujerumani la Kicker, lilimtaja Kaka kama mchezaji bora wa dunia akifuatiwa na Cristiano Ronaldo na Ronaldinho ambaye kwa sasa anachezea klabu ya Ac Milan.
Tuzo nyengine ambazo Kaka amezinyakua hadi sasa ni pamoja na ile ya Revista Placar Bola de Ouro mwaka 2002, Mchezaji bora wa Campeonato kwa mwaka 2002 pia. Alichukua pia tuzo ya mchezaji bora wa Kombe la CONCACAF kwa mwaka 2003.
Mwaka 2005 alichukua tuzo ya kiungo bora wa UEFA Champions League, na mwaka 2006 alinyakua tuzo ya mchezaji bora wa kigeni kwenye ligi ya Seria A nchini Italia.
Haikuishia hapo tu, Kaka alichukua tuzo ya mchezaji bora wa dunia wa Fifpro kwa mwaka 2007 na pia mshambuliaji bora wa ligi kuu barani ulaya kwa mwaka huo huo wa 2007.
Alipewa tuzo ya mpira wa dhahabu kwenye kombe la dunia la klabu, pia alitunukiwa tuzo ya kampuni ya Toyota na ile ya Ballon d’Or- yote hiyo ikiwa ni mwaka 2007.
Huyu ni kiungo mahiri wa mabingwa wa soka Ulaya na dunia nzima kwa ujumla, ambaye licha ya kuibuka mchezaji bora wa Ligi ya Mabingwa Ulaya, pia ametwaa tuzo ya uchezaji bora wa dunia mwaka 2007.
Hivyo, ingawa kila mchezaji amepata mafanikio kulingana na alivyojituma na kujaliwa na Mwenyezi Mungu, lakini huyu ndiye aliyefanikiwa zaidi, japokuwa kuna wengine waliofuatia.
Hao ni kama Christian Ronaldo wa Manchester United ya nchini Uingereza, Samwel Eto’o wa Barcelona ya Hispania, Didie Drogba Chelsea, Fernando Torres wa Liverpool pamoja na Raul Gonzalez wa Real Madrid.
Baada ya kutangazwa kuwa mchezaji bora wa dunia kwa mwaka huo wa 2007, Kaka alikaririwa akisema kuwa:
“Namshukuru Mungu kwa kuwa karibu nami, namshukuru mke wangu, mwanangu na kikosi changu cha Ac Milan pamoja na mashabiki wote wa Ac Milan na Brazil kwa kufanikisha kushinda tuzo hii,” a
Kaka alisema pia, kibinadamu unaweza kumwomba Mungu hiki na kile, lakini kwa mapenzi ya Mungu, anaweza kukujalia zaidi hata ya kile ulichoomba.
Nyota huyu anamaanisha kuwa, yeye aliomba siku moja aje kuwa mchezaji mahiri, lakini Mwenyezi Mungu amemjalia zaidi hata ya alichoomba.
Katika dirisha dogo la usajili la Januari mwaka huu wa 2009, Kaka aliweza kukataa mabilioni ya klabu ya Manchester City ya nchini Uingereza baada ya klabu hiyo kutaka kumchukua kwa kitita cha pauni milioni 100.
Endapo mchezaji huyo angekubali dau hilo, ndio angekuwa mchezaji wa kwanza kununuliwa kwa pesa nyingi kwenye historia ya wachezaji walionunuliwa kutokea ligi kuu nchini Italia.
Katika maisha yake ya kawaida, Kaka ni mtu aliyeokoka na anampenda mungu kikweli. Mara nyingi kwenye mechi ambazo anacheza na kufanikiwa kufunga goli, ndani huvaa fulana inayoonyesha maneno ya mungu.
Kwa mfano mwaka 2005 wakati timu yake ya taifa ya Brazili ilipocheza na Argentina kwenye mchezo wa kirafiki, Kaka aliionyesha fulana yake ya ndani iliyokuwa na maneno "JESUS LOVES YOU' baada ya timu yake kuibuka na ushindi wa magoli 4-1.
Mwaka 2005 Kaka alifunga ndoa na Caroline Celico mwenye umri wa miaka 23 kwa sasa, ndoa ilifungwa huko nchini Brazili kwenye mji wa Sao Paulo. Hadi sasa wanandoa hawa wamebahatika kuwa na mtoto mmoja Luca Celico Leite aliyezaliwa Juni 10 mwaka 2008.
Jina la Kaka alilipata kwa kaka yake anayeitwa Rodrigo ambaye pia ni mwanasoka, kwa sasa anachezea klabu ndogo huko nchini Brazili ya Alphavile- alizoea sana kumuita "Caca", baadae akawa anamuita Ricky na mara ikabadilika na kuitwa KAKA jina lililozoeleka hadi hii leo kwenye ramani ya soka ulimwenguni kote.
KAKA NA TIMU YA TAIFA YA BRAZILI
Kaká alianza kuonekana kwenye kikosi cha Brazil mwaka 2002, siku ilipokutana na Bolivia.
Alikuwa mmoja wa wachezaji walioiwezesha timu ya Brazil kuchukua Kombe la Dunia mwaka 2002 kwa kuifunga Ujerumani 2-0 katika fainali hizo.
Akiwa chini ya kocha Luize Felipe Scolari kipindi hicho, Kaka aliweza kucheza kwa dakika 25 tu kwenye michuano hiyo hiyo wakati Brazili ilipokutana na Costa Rica.
Mwaka 2003, Kaká aliteuliwa kuwa nahodha katika michuano ya Kombe la Dhahabu, ambako Brazil ilimaliza ikiwa bingwa huku Kaka akiwa wa pili kwa ufungaji kwa kupiga mabao matatu.
Juni 29, 2005, aliisaidia timu yake kuitandika Argentina 4-1 katika mechi ya CONCACAF.
Mwaka 2004, Kaka alimaliza huku akipigiwa kura na kutwaa tuzo ya mchezaji bora wa dunia wa mwaka huo.
Mwaka 2006, Kaká aliipaisha timu yake kwa kuifungia bao la pekee katika mechi ya ufunguzi walipoifunga Crotia katika michuano ya fainali za Kombe la Dunia mwaka huo.
Kaka, aliendelea kuwa mchezaji mzuri hadi pale walipoondolewa na timu ya Ufaransa kwenye robo fainali za Kombe la Dunia.
Septemba 3, 2006, aliifungia Brazil bao ambalo liliwajengea heshima na kufuta uteja kwa timu ya Argentina, iliyo pia Amerika ya Kusini.
Mei 12, 2007, Kaka aliachwa kwenye kikosi cha Brazil kilichoshiriki Kombe la Copa Amerika baada ya nyota huyo na Ronaldinho Gaucho kusema walihitaji kupumzika.
Baada ya kikosi hicho cha timu ya taifa kuchukuliwa na aliyekuwa beki wa zamani wa timu hiyo Carlos Dunga, aliamua kumrejesha Kaka katika kikosi chake baada ya kupigiwa kelele na mashabiki.
Kaká, aliitwa kwenye kikosi hicho na kucheza dakika 70 siku Brazil ilipotoka sare ya 1–1 katika mechi ya kirafiki dhidi ya Uingereza Juni mwaka 2008.
Alikuwamo pia katika kikosi cha Brazil ambacho Juni 5, kilitoka sare ya bila kufungana na Uturuki.
Kaka ni muumini mzuri wa Kikristo, anayeabudu madhehebu ya Evangelical Christian, tangu akiwa na umri wa miaka 12.
Mwaka 2002, katika fainali za Kombe la Dunia, Kaka aliwahi kuvua jezi yake na kubaki na fulana iliyokuwa na maandishi yaliyokuwa na ujumbe wa kumtukuza Mungu ‘God is faithful’.
Mbali ya soka, Kaka ni mpenzi mkubwa wa muziki wa Injili na mara nyingi husoma Biblia katika kujifunza neno la Mungu. Kwa maneno mengine, Kaka ni mlokole.
Hivi sasa mchezaji huyo anachezea klabu ya Ac Milan ya nchini Italia chini ya kocha Carlo Ancelotti, pia yupo kwenye kikosi cha timu yake ya taifa ya Brazili ambaco kinawania kufuzu kucheza la dunia ambalo kwa mara ya kwanza katika historia ya soka duniani linafanyika barani Afrika kule Afrika Kusini.
Huyo ndie Ricardo Izecson dos Santos Leite maarufu kama Kaka, mchezaji mwenye mafanikio zaidi ambaye anajivunia kumpenda mungu kutokana na wokuvo alioupata tangu akiwa na umri wa miaka 12.
Simu: 0719000010

E-mail: jmihiko@yahoo.com

KARIBUNI TANGA WADAU.

Moja kati ya watu ambao nawaheshimu sana katika maisha yangu, ni baba yangu mzazi Hammie Rajab ambaye kwa kweli amekuwa akinionyesha njia nzuri ya kuishi maisha bora hapo baadae. Kupitia vitabu ambavyo ameandika kama 'SANDA YA JAMBAZI', ' KAMLETE AKIBISHA MLIPUE', 'MLIMA KOLELO' pamoja na novo ambayo inasomwa nchini Kenya hivi sasa 'REST IN PEACE DEAR MOTHER' ni miongozi mwa vitabu vilivyonipa msukumo mkubwa wa kuingia kwenye ramani ya uwandishi ili hali kuendeleza heshima yake kwenye fani hii.

Nawakaribisha ndugu, jamaa, marafiki pamoja na kila mwenye kuvutiwa na blog hii, tubadilishane mawazo ili tuweze kumshinda mdudu UJINGA katika nchini yetu.

Kwa sasa nafanya kazi Redio Mwambao Fm Sauti Ya Tanga, nipo hapa kama mtangazaji, mwandishi wa habari na kusimamia productio za redio.

Nimeshaandika hadithi pia, ila kwa sasa zaidi ya kuwa mmoja wa watu wanofanya vizuri mkoani Tanga kupita Redio- lakini pia naandika makala kwenye gazeti la Tanga Yetu ambalo lipo hapa Tanga.

Karibuni Wote, ila huu ni mwanzo tu. Kila kitu kitakaa sawa mambo yakiwa mazuri zaidi.